Leo Oct 31 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli, ameanza ziara ya Kiserikali ya siku mbili nchini Kenya kwa
mwaliko wa Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta.
Rais
Dr.Magufuli anatarajiwa kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Jomo Kenyatta Jijini Nairobi majira ya saa nne asubuhi na baadaye
kupokelewa rasmi na mwenyeji wake Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi
ambako viongozi hao watafanya mazungumzo.
Pamoja na
kufanya mazungumzo na mwenyeji wake, Rais Magufuli atakwenda kutoa
heshima katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Kenya Hayati Mzee Jomo
Kenyatta na pia anatarajiwa kuhudhuria dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa na
mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta Ikulu Jijini Nairobi
Katika
ziara hii Rais Dr. Magufuli anatarajiwa kutembelea kiwanda cha maziwa cha
Eldoville kilichopo Karen Jijini Nairobi, na pia anatarajiwa kuzindua
barabara ya Southern By-pass iliyopo Jijini Nairobi.
No comments:
Post a Comment