Msanii wa muziki wa kurap, Mr Blue amesema hahitaji kuwa na meneja wa kumsaidia katika kazi zake za muziki kwa kuwa tayari alishawahi kuwa na mameneja zaidi ya watatu ambao hawakumpatia mafanikio yoyotee.
Mr.blue ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Mboga Saba’ amesema alikuwa hawezi kuishi kwenye tasnia ya muziki bila kuwa na meneja lakini kutokana na kuona mchango wao kwake haukuzaa matunda akaamua kuachana nao kabisa
Rapa huyo kwasasa anaitaji ushauri wa wadau namna ya kuboresha kazi zake” Mr Blue.Hivi sasa pamoja na AliKiba wameshiriki kusapoti ngoma ya Abby Skills inayokwenda kwa jina la Averina , ambapo Abby Skills amewataka mashabiki kumuunga mkono ili arejee vyema kwenye game kama zamani.
No comments:
Post a Comment