MOJA YA BARUA ILIO ANDIKWA NA YANGA
Siku chache baada ya kocha mkuu wa klabu ya Dar es Salaam Young Africansi Hans van Pluijm ajiuzulu nafasi yake hiyo, leo October 28 2016 klabu ya Yanga imemuandikia barua ya kumuomba abadili maamuzi yake ya kujiuzulu na arejee kazini kama kawaida.
Baada ya uongozi wa klabu ya Yanga kupitia kwa kaimu katibu mkuu wake Baraka Deusdedit pamoja na waziri wa mambo ya ndani ya nchi ambaye pia ni shabiki wa Yanga na mwanachama mh.Mwigulu Nchemba, wamemuomba kocha Hans Pluijm atengue uamuzi wake wa kujiuzulu na kurudi kazini kama kawaida.

No comments:
Post a Comment